Header AD

HADITHI: NAYAPENDA MAISHA LAKINI MAISHA HAYANIPENDI



                                                  

Story:NAYAPENDA MAISHA LAKINI MAISHA HAYANIPENDI
SEHEMU YA (2)
MWANDISHI: ZABRANCO

Ghafla, milio ya risasi na magurumeti ikaanza kusikika ikitokea upande wa kaskazini magharibi mwa kitongoji cha watengwa area zone, wale wapiganaji wakampiga risasi mama wa herera kisha  wakapanda gari lao wakatokomea ndani ya msitu, herera akabaki pale chini huku akiwa Analia kwa majonzi ya kuwapoteza wazai wake huku akiwa anaona kwa macho yake, herera akaanza kujiburuta taratibu ili kuelekea pale maiti ya baba yake na mama yake ilipokua imelala
, lakini kila herera alipokua anataka kusimama alikua anajikuta akishindwa kwa sababu alikua kaumia mbavu kutokana na lile teke alilopigwa na yule mkuu wa kile kikundi cha waasi. Herera akajiburuza hadi pale walipokua wamefia wazazi wake kisha akaisogelea maiti ya baba yake chozi la huzuni likawa linatanda kwenye uso wa herera, akaifumba macho maiti ya baba yake kisha akasimama  akaisogelea maiti ya mama yake iliyokua imetapakaa damu kutokana na risasimfururizo alizopigwa maeneo ya kifuani.


              Herera akaikumbatia maiti ya mama yake huku akiwa Analia kwa machungu, akaifumba macho ile maiti huku akiwa anawaza ni jinsi gani atawazika wazazi wake kwa hua alikua kaumia vibaya mbavu zake hakua na uwezo wa kusimama wala kutembea akaona njia pekee ya kusaidiwa ni kupiga kelele kuwaita majirani, lakini akwaza kua watu wa ‘watengwa  area’ hua hawatoki nje kipindi wanaposikia milio ya risasi kwenye kitongoji chao, herea akajaribu kuita watu waje kumsaidia akaita mara tatu kwa sauti ya juu lakini hakuna hata mmoja aliyejitokeza kuja kumsaidia hakukata tamaa akaendelea kuita kwa sauti ya juu huku akisema kua wasiogope tayari waasi wameshaondoka, aliposema hivo ndipo watu wakaanza kuchungulia kwenye madirisha ya nyumba zao, kweli wakamuona herera akiwa amekaa pale nje huku kwa pembeni yake kuna maiti mbili. Akatoka mwanaume mmoja akamsogelea herera pale alipokua amekaa, kisha watu wakazidi kuchomoza wakitokea ndani ya nyumba zao kama kuku waliofunguliwa kutoka nje y a banda lao, wakamzunguka herera huku wakisikitika kwa njisi zile maiti za majirani zao zilivyokua zimeraruliwa kinyama. Wakachukua kanaga wakazifunika zile maiti kisha wakazichukua na kuzipeleka kwenye nyumba ya kina herera iliyokua imeezekwa kwa kutumia makuti kwa kua nyuimba yao ya awali ilipigwa bomu miaka miwili iliyopita pale ambapo kulikua na mapigano makali kati ya waasi na wanajeshi wa serikali ya nchi ya ‘RED ZONE’.


         Nyumba ya kina herera ilikua ikidhihirisha kua watu wa kitongoji cha ‘watengwa area’ ni masikini wakutupwa kutokana na madhara ya vita amabayo imekua ikitokea kwa miaka mingi sana. Watu wakakubaliana kua inabidi wazizike maiti za wazazi wa herera, siku iliyofuata mazishi yakafanyika kwenye shamba la kina herera lilokua limezagaa mahindi yaliyoharibiwa vibaya kutokana na waasi kupitisha magari yao ya kivita ndani ya mashamba ya watu wa kitongoji cha watengwa area. Wazazi wa herera wakazikwa kwenye lile shamba kisha watu wakatawanyika huku herera akabaki kua yatima akiwa hana shangazi wala mjomba wala ndugu yeyote kwa kua ndugu zake wengi walishauawa kutokana na vita ndani ya nchi ya ‘RED ZONE’, huku ndugu engine wakiwa wamekimbia na kuelekea nchi za mbali ambako walihisi kua watakua salama.




                                   Herera akiwa maekaa pale pembezoni mwa bahari huku akiwa anavuta kumbukumbu ya maisha aliyopitia hadi hapo alipofikia kua mtu mziam akiwa amezaliwa kwenye nchi yenye vita hadi amekua mtu mzima akiwa na watoto wawili lakini bado vita inaendelea, akakumbuka jinsi alivyobakwa na wanajeshi wa jeshi la kulinda Amani la nchi ya ‘RED ZONE’kwa kua alikua nib inti mwenye mvuto sana ilitokea wanajeshi wanne waliokua wamekuja kufanya patro katika kitongoji ch watengwa area, kipindi hicho herera alikua na umri wa miaka kumi na nane, siku moja akiwa anatoka kisimani kuchota maji, kisima kilikua umbari wa kilometa mbili kutokana na uhaba wa maji ulio kikumba kitongoji cha ‘watengwa area’.



                     Herera akiwa na rafiki zake wakitoka kisimani kuchota maji, walikutana na wanajeshi nane wa kikosi cha serikali wakiwa katika doria wale wana jeshi wakawasimamisha kina herera na rafiki zake wawili kisha mmoja wa wanajeshi akasema, “ Wewe binti mbona mzuri sana utazani hujazaliwa kwenye vita!”, kisha akamsogelea herera akamuuliza kua anaitwa nani hereara akajibu kwa woga “naitwa herera”. Yule mwanajeshi akatabasamu kisha akamshusha herera ile ndoo aliyokua kabeba kichwani.                                                    
               Kisha akamsogeza herera pembeni akaanza kumshawishi kua wakafanye mapenzi kwenye vichaka vilivyokua pale pembeni, lakini herera akakataa, yule mwanajeshi akakasirika akamshika herera mkono kw anguvu kisha akampeleka pale kwa wenzake akasema “aseeeee!mazee eti hiki kimanzi kinagoma kufanyiwa, sasa ngoja tukifunze adabu”. Wale wanajeshi wakawatishia herera na wanzake kua wasipokubali kufanya mapenzi watawaua, wale wanajeshi wakawashika kwa nguvu wakaambia atakaye piga kelele watampiga risasi, wakapeleka ndani ya vichaka……………..(nini kilitokea?, usikubali kupitwa ingia www.duniamtandaoni.blogspot.com).
HADITHI: NAYAPENDA MAISHA LAKINI MAISHA HAYANIPENDI HADITHI: NAYAPENDA MAISHA LAKINI MAISHA HAYANIPENDI Reviewed by Unknown on Novemba 21, 2016 Rating: 5

Hakuna maoni

Post AD

Propellerads