Header AD

Trump amteua mkwe wake kuwa mshauri mkuu Marekani


Jared Kushner akiwa na mkewe binti wa TrumpHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionJared Kushner na mke wake

Rais mteule wa Marekani Donald Trump amemteua mkwe wake Jared Kushner, kuwa mshauri mwandamizi wa Ikulu ya nchi hiyo.
Kushner mwenye umri wa miaka 35 ambaye amemuoa binti mkubwa wa Trump, Ivanka, alifanya kazi kubwa wakati wa
kampeni za uchaguzi, zilizomuwezesha Trump kushinda.
Majukumu ya kazi yake yanatarajiwa kuhusika na masuala ya sera za nje na ndani ya nchi, ikiwemo masuala ya biashara na Mashariki ya Kati.
Uteuzi huo hauhitaji kuthibitishwa na bunge la seneti.
Lakini hata hivyo baadhi ya wachambuzi wanahoji kama uteuzi huo utakiuka sheria ya kupinga upendeleo wa undugu katika ajira.
Jared Kushner hata chukua mshahara kwa uteuzi huo wa Ikulu ya Marekani na itampa nafasi ya kumfanya kuwa huru na maslahi ya shughuli zake za kibiashara.
Trump amteua mkwe wake kuwa mshauri mkuu Marekani Trump amteua mkwe wake kuwa mshauri mkuu Marekani Reviewed by Unknown on Januari 10, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Post AD

Propellerads