Header AD

Mahakama kuu ya China: Trump ni adui wa utawala wa sheria duniani

Mahakama Kuu ya China imemtaja Rais Donald Trump wa Marekani kuwa adui wa utawala wa sheria duniani.
Taarifa iliyotolewa na mahakama hiyo kupitia jaji mkuu wa nchi hiyo imesema kuwa, misimamo inayotolewa na rais huyo ambayo imesababisha changamoto nchini Marekani,
imekuwa chanzo cha kuibuka uadui dhidi ya sheria. Aidha imeongeza kuwa, misimamo ya rais huyo imeinyima mahakama ya Marekani uhuru wake katika maamuzi.

Mahakama kuu ya China

Hii ni katika hali ambayo Wizara ya Sheria nchini Marekani inajaribu kuchunguza hukumu zilizotolewa na mahakama tisa za nchi hiyo katika kupinga misimamo ya Rais Trump. Mahakama hizo zimesisitiza kuwa, rais huyo hana haki ya kuwazuia raia Waislamu kuingia Marekani na hivyo viwanja vyote vya ndege na mipaka ya nchi hiyo vinatakiwa kufunguliwa kwa ajili ya kuingia watu hao.

Rais Donald Trump wa Marekani

Siku chache zilizopita pia, Joe Chiang, Mkuu wa Mahakama Kuu ya Watu wa China aliwataka majaji wa nchi yake kutupilia mbali mienendo isiyo sahihi ya Wamagharibi sambamba na kuwataka wasiruhusu kuingiliwa kisiasa uhuru wa vyombo vya mahakama nchini humo
SOURCE: ParsTODAY

Mahakama kuu ya China: Trump ni adui wa utawala wa sheria duniani Mahakama kuu ya China: Trump ni adui wa utawala wa sheria duniani Reviewed by Unknown on Februari 09, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Post AD

Propellerads