Header AD

Jina la wizara latumika kutapeli wafanyabiashara

Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) wilayani hapa, umesema kumeibuka matapeli wanaotumia jina la Wizara ya Maliasili na Utalii kuwatapeli wafanyabiashara wa mazao ya misitu.

Meneja wa TFS Wilaya ya Kibaha, Peter Nyahende ametaja eneo lililoshamiri kwa utapeli wa aina hiyo kuwa ni Barabara Kuu ya Morogoro- Dar es Salaam, hususan Maili Moja na kwamba watu hao  wamekuwa wakijiita Paruanji.

Nyahende alisema watu hao pia hujifanya ni maofisa misitu na kuwatapeli wafanyabiashara wasiofuata utaratibu wa usafirishaji  na kuchukua fedha badala ya kuwafikisha kwenye vyombo vya dola.



Alisema wafanyabiashara hao bila kujua wametapeliwa, hukumbana na mkono wa sheria baadaye wanapokutana na maofisa Maliasili halisi.
Jina la wizara latumika kutapeli wafanyabiashara Jina la wizara latumika kutapeli wafanyabiashara Reviewed by Unknown on Oktoba 21, 2016 Rating: 5

Hakuna maoni

Post AD

Propellerads