Header AD

NIKOHURU BLOG#Serengeti Boys yapata ushindi dhidi ya Congo Brazzaville


img_3395
Timu ya Serengeti Boys ya vijana chini ya umri wa miaka 17 imepata ushindi wa mabai 3-2 dhidi ya Congo Brazzaville katika hatua ya tatu kuwania kufuzu michuano ya Afrika kwa vijana
itakayofanyika mwakani AFCON 2017 Madagascar.
Magoli ya Serengeti Boys yalifungwa na Yohana Mkomola aliyefunga mawili na Issa Makamba, wakati magoli ya Congo yalifungwa na Langa Percy kwa mkwaju wa penati na Bopoumela Chardon.
Mgeni rasmi alikuwa ni Nape Nnauye ambaye ni waziri wa utamaduni na michezo aliahidi pia kununua bao moja kwa Sh 500,000 na atalipa fedha hizo kadiri ya idadi ya mabao hata kama yatafika 10 hivyo gharama yake itakuwa Sh 5,000,000. Kuna wabunge na viongozi wengine waliahidi kutoa fedha zaidi.


Timu hizo zinatarajiwa kurudiana Oktoba 2 ambapo mshindi wa hapo atasonga mbele kwa kufuzu moja kwa moja katika michuano hiyo ya vijana.
NIKOHURU BLOG#Serengeti Boys yapata ushindi dhidi ya Congo Brazzaville NIKOHURU BLOG#Serengeti Boys yapata ushindi dhidi ya Congo Brazzaville Reviewed by Unknown on Septemba 19, 2016 Rating: 5

Hakuna maoni

Post AD

Propellerads