Header AD

Trump : 'Namheshimu Rais wa Russia Vladimir Putin, lakini…'

Rais Donald Trump - Rais wa Russia Vladimir Putin
Rais Donald Trump amesema ijapokuwa “anamheshimu”
 Rais wa Russia Vladimir Putin sio lazima kuwa
 mtangamano wao utadumu.
“Lakini nasema ni bora kushirikiana na Russia kuliko vinginevyo
. Na kama Russia itatusaidia katika kupambana na kundi la
 Islamic State, ambayo ni vita kubwa, na ugaidi wa kiislamu dunia 
nzima—
hilo ni jambo zuri,” Trump ameliambia shirika la Televisheni
 la Fox News katika mahojiano yake ambayo yatatangazwa Jumapili.
“Je nitaweza kushirikiana naye? Sina wazo lolote kuhusu hilo.”
Udhalimu wa Putin
Alipoulizwa kuhusu mauaji alioyafanya Putin siku za nyuma, na jinsi gani Trump angeweza kumheshimu
 hata baada ya kujua historia yake, Trump ameifananisha Russia na Marekani.
“Kuna wauaji wengi. Sisi pia tunao wauaji wengi. Unafikiria nini? Nchi yetu haina makossa? amesema
 hayo, kwa mujibu wa sehemu ya maelezo hayo yaliyo patikana kutoka katika mahojiano yake na
 Fox News siku ya
 Jumapili.
Kiongozi wa Baraza la Seneti
Mitch McConnell
Mitch McConnell
Akijibu juu ya maoni haya ya Trump kwenye televisheni ya CNN, kiongozi wa wengi katika Baraza la 
Seneti Mitch McConnell amesema yeye hafikirii “tunaweza kuilinganisha” Marekani na Putin.

Mashirika ya kipelelezi Marekani yameishutumu Russia kwa udukuzi wa kompyuta zilizokuwa zikitumiwa na
 Chama cha Demokratik kama njama ya kampeni pana za Russia kuvuruga uchaguzi wa urais wa Marekani.

Kabla ya kuchukuwa madaraka, Trump alirejea mara nyingi kudadisi taarifa za jumuiya ya kipelelezi. Lakini
 ukosoaji wake umesita kwa muda sasa. Bado, rais ameendelea kusema hadharani kwamba yuko
 tayari kwa mahusiano bora na Moscow.
Mazungumzo ya Trump na Putin
Trump na Rais wa Russia walikuwa katika mazungumzo ya simu siku ya Jumamosi katika kile
 White House ilichokiita kama “ ni mwanzo muhimu katika kuboresha mahusiano kati ya Marekani na
 Russia jambo ambalo lilikuwa linahitaji hatua hiyo.”
Vipande ya mahojiano hayo vina swali linalo ongelea agizo la Trump kuhusu uchunguzi wa wizi wa 
kura katika uchaguzi wa urais Novemba.
Madai dhidi ya Hillary
Hillary Clinton
Hillary Clinton
Trump amedai mara nyingi kuwa wahamiaji haramu walopiga kura wamemzuilia kupata kura ya
 umaarufu. Trump alishinda kura za wajumbe “Electoral College” lakini alipoteza kura za umaarufu kwa
 idadi ya kura
 milioni 2.9 ambazo zilichukuliwa na mgombea wa Demokratik Hillary Clinton katika uchaguzi mkuu mwaka
 jana.
“Nataka niwaambie unapoona wahamiaji haramu – watu ambao sio raia na wapo katika usajili wa 
kupiga kura,” Trump amesema. “Utawaona wahamiaji haramu, wako watu waliokwisha kufa, una haya
 yote, ni hali mbaya sana, kwa kweli ni mbaya.”

Hata hivyo maafisa wa uchaguzi ambao walizichambua kura za Novemba 8 wanasema hakukuwa na dalili
 yeyote ya wizi wa kura, kwa kweli sio katika kiwango kinachoelezewa na Trump.

CREDIT: VOA

Trump : 'Namheshimu Rais wa Russia Vladimir Putin, lakini…' Trump : 'Namheshimu Rais wa Russia Vladimir Putin, lakini…' Reviewed by Unknown on Februari 06, 2017 Rating: 5

Hakuna maoni

Post AD

Propellerads